MISHE-BOY

News | Big Fizzo aomba kufanya Collabo na Nay Wa Mitego wa Bongo Fleva

Nyota wa muziki wa Buja Fleva, Big Fizzo boss wa lebo ya Bantu Bwoy alifunguka mbele ya waandishi wa habari katika press conference ya Nay Wa Mitego nchini Burundi, Agosti 09, 2018 kwenye ukumbi wa Lacosta Beach kwa kuomba kufanya collabo na Nay Wa Mitego.

Katika maojiano na waandishi wa habari msanii mwenye vituko kutoka Tanzania, Nay Wa Mitego ameanza kwa kumwagia sifa nyingi Big Fizzo kwa kusema kwamba anapenda sana kazi za Fizzo na anampenda sana huku akiongeza kusema kuwa mara nyingi anapenda kusikiliza kazi zake.

Aidha, Big Fizzo alichukua mda wa kumshukuru Nay Wa Mitego na mujeshi mwenzie ambae ni T Max na kusema,

"Asante sana Nay kwa kukubali kazi zangu nami pia nakubali sana kazi zako na ningependelea nifanikishe kufanya kazi na wewe endapo utakubali ombi langu, nakuomba sana collabo hiyo ifanyike ninanimani itapendeza zaidi".

" Usijali ninaimani kwamba hakuna ugumu wowote wa kufanya collabo hiyo kwa sababu tayari nimewasili Burundi na Meneja wangu yuko njiani pindi atakapo fika tu tutaimaliza na collabo hiyo bila shaka itakuwepo tu", alijibu Nay Wa Mitego

Hakuna maoni