MISHE-BOY

News | Hatimaye waombana msamaa baada ya kila mtu kusema ya moyoni

Msanii wa muziki, Big Fizzo na mtangazaji wa kituo cha radio Rema FM, Ismail Niyonkuru walimaliza bifu yao ya mda mrefu Agosti 09, 2018 kwenye ukumbi La Pirogue.

Hakuna hasiye faham mzozo uliokuwepo kati ya Ismail na Big Fizzo na hakuna aliamini kama kuna siku wawili hawo siku moja watarudi kuwq pamoja na kuelewana.

Baada ya kutoka uwanja wa ndege Bujumbura kumpokea rapa T Max akitokea Ulaya, Msanii Happy Famba aliwaomba watangazaji kukaa sehemu moja na kujadili kuhusu muziki wa Burundi kwa neno la kipi kifanyike ili muziki wa Buja Fleva usonge mbele.
Kila mtu aliongea ya moyoni na ila kikao icho kimekuja kugeuka cha watu wawili pale ambapo umoja alichukua mda wakuongea ya moyoni na kuweka wazi tatizo yao inayoleta utata mda mrefu mpaka imeamia kwa mashabiki wa muziki.

"ili muziki wa Burundi usong mbele inabidi kwanza watangazaji wafanye kazi ipasavyo bila kujali pesa au ushkaji. Watangzaji wengi wanatafuta wawe ma staa kupitia jina la wasanii. hamjuwi tulipo toka mpaka tunafikia levo kama hii, sasa acheni kupoteza mda kwa kupinda kazi zangu kuliko kuongelea mazuri yangu. sikatai kuongelewa ila ongeo ukweli bila kuongeza uongo ndani yake. mara nyingi siongelewi mpaka natamani kuzua chochote kile ili niongelewe ila watangazaji wengi wanaongea mabaya ya mtu mazuri wanayafumbia macho. Ismail nilikua sikufahamu ila nafurahi Famba katukutanisha hapa nilikua nakusikia tu ila ujuwe unafanya kazi nzuri ila why Fizzo tu unamuongelea vibaya hivi hakuna mazuri yangu unayajua?", Alisema Big Fizzo

"Najua hakuna mkamilifu chini ya jua nina mabaya yangu na pia mazuri ila mimi nazidi kufanya kazi yangu ila nakumbuka niliwahi kukutangazia sana mpaka kiongozi wa radio alitaka kuninyima mshahara ila baadae umenilipa matusi na kunitumia watu waje kunipiga ila yote tisa mimi naendelea kufanya kazi, sina bifu na wewe Fizzo acha tufanye kazi na wewe ufanye kazi ipasavyo".

" Eti nikutumie watu wakupige? hahahahaha sijawai kutuma watu ila nawakataza watu ambao wana hamu ya kukupiga, mimi mwenyewe naweza kukupiga sio mpaka nikutumie watu Ismail. Ila najua kama wimbo wangu umekupa chata dogo langu ( ismail) hahahahah ila nakuomba sana pindi nikikojoa barabarani tangaza kama nilikojoa bila kuongeza mengine ya uongo", Aliongeza Big Fizzo


Aidha, Msanii Happy Famba alichukua mda wakuweka mambo sawa mpaka kila mmoja (Fizzo na Ismail) akasema kwamba hana matatizo na mwenzie mpaka wawili hawo wakapeana tano ishara ya upendo kati yao na kuchukua mda wa kuongea huku wakitabasam.

Hakuna maoni