MISHE-BOY

je unajua wachezaji maharufu sana ambao awachezeyi timu yao ya taifa ya brazilia?

timu ya taifa ya brazil mwaka huu ndio timu inayo pewa pato kubwa sana kwa kuchukuwa kombe la dunia ambao inadhuru nchini mwao Brazil, timu ya brazil inayo wachezaji wazuri sana kama Neymar, Thiago Silva, Hulk, David Luiz ao pamoja na Ramis, ukitizama wachezaji wote na listi ya kumi na moja ni vigumu sana kupanga ndio sababu inayo pelekeya wachezaji wengine wanao na asili ya brazil kugeuza na kuchezea nchi zingineo ambazo zinawahitaji.
kwa uchunguzi wetu  tunawapa wachezaji 11 ambao ni wachezaji marufu sana kwenye ligi mbalimbali ya ulaya.
PEPE
1. Pepe : kwa  jina lake la ukweli alio pewa na wazazi wake ni Képler Laveran Lima Ferreira, ni beki wa Real Madrid ya Ispania, amezaliwa 1983 , Maceió nchini Brazil, matarajio yake ilikuwa ni ya kuichezea timu yake ya taifa ya Brazil ila ndoto yake aikutimia na akaweza kujiunga na timu ya taifa ya Ureno (Portugal) mwaka wa 2007.

 2.Thiago Motta: amejulikana sana kwenye ligi ya ufaransa kwenye timu kubwa sana Paris-Saint-Germain, kwajina lake halisi ni Thiago Motta Santon Olivares, amezaliwa 1982, São Bernardo do Campo mjni São Paulo nchini Brasil. ameanza kazi yake ya mpira nchini Brazil ila wazaji wake ni wenyeji wa Italia kwani anachangwa, amependelea kuchezea timu yake ya taifa ila akuwahi kuhitwa kwenye orodha ya Brazil.ndipo ameamua kujiunga na timu ya Italia toka mwaka wa 2011.
Thiago Alcantara
 huu ndiye baba mzazi wa mchezaji Thiago Alcantara kwajina maharufu Mazinho

3.Thiago Alcantara : kwa upande wake amechaguwa kuichezea Ispania pali ya nchi yake ya Brazil, amezaliwa Italia, San Pietro Vernotico na ni mtoto wa kwanza wa mchezaji wazamani wa Brazil Mazinho, Thiago amewahi kuchezea Ispania ya kocha Vicente del Bosque mwaka wa 2011 tarehe  10/10 kwenye machi ya kirafiki dhidi ya Italia. kwa bahati mbaya mwaka huu akuitwa kushiriki kwenye kombe la dunia.



Cacau
4.Cacau: kwa jina lake la ukweli ni Claudemir Jerônimo Barrettoalmaarufu kama Cacau, amezaliwa tarehe 27/3/1981 mjini Sao Paulo, ila ameenza kazi yake ya soka nchini Ugerimani katika klabu ya FC Nuremberg mpaka sasa ajawahi kucheza ligi nyingine isipokuwa ya ligi ya Ugerimani almaarufu kama Bundesliga, na ikamupelekea kujiunga na timu ya taifa ya Ugerimani(Allemagne) kwa sasa amewahi kuitwa mara 25 kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Ugerimani almaarufu kama  nationalmannschaft.
Marcos
5.Marcos Andrès Gonzalez Salazar :  huu ndiye mchezaji ambae amejulikana sana na watu wengi barani ulaya.  amezaliwa mwaka wa 1980 mjini Rio Janeiro ila kwa sasa anaaendelea na kuitangaza nchi ya Chili upande waulinzi. ameanza kazi yake ya soka nchini Chili katika klabu ya Universidad, mwaka wa 2012, kwasasa amerudi nchini mwake Brazil katika timu ya Flamengo.

Alves Da Silva
6.Eduardo Alves Da Silva : ni mchezaji wa zamani wa Arsenal pia ila kwa sasa anacheza katika timu ya taifa ya Croatia ndiyo timu ambao ameichaguwa uku akigombaniwa pia na timu ya taifa ya Ukraine na amezaliwa mjini Rio Janeiro.
Giovani dos Santos


7.Giovani dos Santos : mchezaji huu amejulikana kwenye klabu ya Barcelona ya Ispania na pia amechagua kuichezea timu ya taifa ya  Mexik, alipendelea kuichezea timu yake ya Brazil kama baba yake mzazi Zizinho. ila kwasasa anatamba na timu ya taifa ya Mexik.
Igor de Camargo
9.Igor de Camargo : Igor de Camargo amezaliwa 12 mei 1983 mjini Porto Feliz nchini  Brésil.  juni 2008, amekabidhiwa urahia wa Ubelgiji kwasababu amecheza miaka nyingi na kuonekana sana kwenye ligi ya Ubelgiji tangu mwaka 2000 na amewahi kucheza machi yake ya kwanza pamoja na timu ya taifa ya Ubelgiji mwaka wa 2009 upande wa ushambuliaji na ameondolewa mwaka wa 2012.
Benny Feilhaber
10.Benny Feilhaber : Benny amezaliwa tarehe 19 januari 1985 katika Rio de Janeiro. Benny amecheza katika klabu ya MLS mwaka wa 2011,  na kwa  namna iyo amegeuka raia wa Amerika, amewahi kukataa wito wa kujiunga na Autriche akaamua kuichezea Etats-Unis.
11.Brandao : huu mchezaji mwenye asili ya Brazil kwajina lake halisi ni Evaeverson Lemos da Silva amezaliwa pia Sao Paul, kwasasa ni mfaransa ila ametaka kujiunga na kikosi cha Ufaransa bahati mbaya akuweza kuwekwa kwenye wale 23 walio pendezwa na kocha Didier Deschamps kwenye kombe la dunia.
12.Diego costa: kwajina lake Diego da Silva Costa, amezaliwa mwaka wa 1988, huu mchezaji amekuwa ameitwa na kamati nzima ya michezo ya brazil mwaka huu ili ajiunge na timu ya taifa ya brazil ila walipo muhoji kocha Scolari amejiu kwamba, Diego ni mchezaji mzuri ila kwa kikosi changu nitaweza kuweka katika wachezaji 23 ila awezi cheza mbele ya Fred. ilo neno limemuuma sana Diego, gafla akapigiwa simu na kocha wa Ispania na kuongea naye na kufikia na makubaliano ya yeye kugeuza urahia nakuichezaea Ispania ata kama akuweza kufanya vizuri kama gisi wapenzi wake walivyo taka kumuona akishamiri..

kwa kusaliti nchi yao ya asili na kuichezea ma taifa nyingine kwa wapenzi wa Selesao wanawaita hawa wachezaji kama ni ma Yuda.  kwa kweli sio ma yYuda kama gisi wanavyo waita ila kwenye soka kila mtu eko na maamuzi yake, kwa mfano wanandugu hawa hapa


Prince Kevin Boatenge ambae ndiye mkubwa anachezea timu yake ya asili na mdogo wake Jerome Boateng anaichezea timu ya taifa ya Ujerimani. hapo akuna uyuda nimaamzi na kesho ao kesho yake utakua kuona mrundi anahichezea nchi nyingine.

Hakuna maoni