MISHE-BOY

Sport | Samuel Eto'o ataja mshindi wa mpira wa Dhahabu ujao

Baada ya kujiunga na klabu yake mpya Qatar Sport, Samuel Eto'o alifunguka  katika mahojiano na wenzetu wa RFI, ambapo alizungumzia mada kadhaa ikiwa ni pamoja na mpira wa dhahabu (Ballon D'or).

Raia huyo wa Cameroon mwenye umri wa miaka 37, aliweka wazi pendekezo yake na kuonesha uchaguzi wake wazi. Eto'o Samuel alisema kwamba angependelea kuona kijana, Kylian Mbappé kushinda Mpira wa Dhahabu na hivyo kuvunja utawala wa Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.
Kumbuka kuwa Samuel Eto'o kamwe hajawai kushinda mpira wa dhahabu, lakini mara nyingi alikuwa anawekwa vizuri na kuwa na matumaini ya kuishinda. Mmoja muafrika kushinda mpira wa dhahabu ni George Weah.

Hakuna maoni