MISHE-BOY

Sport (Tetesi) Jackson Baransananikiye anyatiwa na klabu nyingi Burundi

Katika tetesi za usajili nchini Burundi, Jackson Baransananikiye wa Flambeau de L'Est mwenye umri wa miaka 23 anaongoza  orodha ya wachezaji wanaowindwa na klabu za Burundi.



Timu 3 zampigia hesabu huku timu ya vitalo ingali na matumaini ya kumnasa, kocha Kanyakore Gilbert tayari kaonesha niya ya kumsajili Jackson.
Itakuwa vigumu Vital'o kushinda hata Musongati FC ya mkoani Gitega na Ngozi City tayari zimeingia kwenye arakati ya kutaka kumsajili mshambuliaji huyo.


Jackson Baransananikiye alijiunga na Flambeau de L'Est kwenye mechi za marudio akitokea Dikhil FC ya Djiboutie  ambapo aliifungia Dikhil bao 12 na Bao 7 pekee akiifungia Flambeau de L'Est.

Flambeau de L'Est ina hofu kubwa kumpoteza mchezaji wao juu ya ushindani kutokana na timu kadhaa kuonesha niya ya kumsajili, kwa mjibu wa timu ya Flambeau de L'Est wameanza mazungumza na mchezaji ya kumuongeza mkataba.

Hakuna maoni