MISHE-BOY

Sport | Ujumbe wa Didier Drogba kwa Mohamed Salah

Nyota wa Yvory Coast, Didier Drogba alimtumia ujumbe Mshambuliaji wa Liverpool Mohamed Salah ambaye aliweka rikodi ya kuwa Mfungaji Bora wa Afrika katika Ligi Kuu ya Uingereza.

Drogba alipost picha  kwenye akaunti yake ya Twitter akiwa pamoja na mshambuliaji wa Misri Salah  ikiongozwa na maneno yafuatayo :

Hatimaye mfungaji bora kutoka Afrika wa @PremierLeague na mmiliki mpya wa rikodi ya bao alifunga Afrika, MONSIEUR@22Mosalah.

Nikukumbushe kuwa Drogba aliwai kuweka rikodi ya kuwa mwana Afrika wa kwanza kufunga bao 29 kwenye Premier League ila rikodi hiyo imevunjwa na Mohamed Salah wa Liverpool kwasasa tayari ana bao zaidi ya 30.

Hakuna maoni