MISHE-BOY

Fiston Abdul Razak kaziwiliwa na Lydia Lydic Academic

ni mchezaji Mrundi na pia anaichezeya timu ya taifa ya Burundi, alipo anza kuichezea klabu ya daraja ya Kwanza ya hapa Burundi na kuonekana mshambuliaje mzuri sana na kuwekwa katika timu ya taifa.
ameichezeya timu ya taifa ya Burundi kwenye michuano ya Chan 2014 na akafanikiwa kuipeleka kwenye fainali ya Chan 2014 timu ya Burundi na akaichezea timu ya taifa kwenye kinyanganyiro ya cecafa nchini Kenya.
ndipo nyota yake imeanza kuonekana inje ya nchi kwa kuichezea timu ya taifa mwaka huu, kwa habari tumezipata kutoka kwake ni kwamba kuna klabu moja wapo ya Kenya ilipenda kumsajili ila mazungumzo ikawa ngumu kidogo kwa upande zote 2 yaani Supa kapa ya Kenya na Lydia Lydic ya hapa Burundi inayo sema kwamba mchezaji eko na mukataba wa miezi 4 na itaisha mwaka huu mwezi wa 4.
tulipo ojiana naye alikua na mengi ya kusema;
Fiston : kwa kweli mi sielewi kama iyo malalamiko ya Lydia Lydic ya kusema kwamba tuko na mkataba nawo kwajili mimi sijawahi kusaini mkataba na Lydia Lydic tangu ni ichezeye, ni kwamba mi nao ( Lydia Lydic) tulikua tunaelewana tu kimudomo yaani kila msimu wa ligi wamekuwa wananipa laki mbili tu bila kuongea kitu na bila kuandikiana fasi ila wa sasa nimekwisha kuwa mchezaji mkubwa inanibidi niwe na mkataba wa klabu yeyote na bahati nzuri nimepata klabu ya Kenya. 

tukumbuke kuwa alipo ulizwa kenya kwajili ya mkataba wake na Lydia Lydic amesema ukweli wake kwamba:
Fiston: niliwaambia tu kama niko free na sina mkataba wowote na Lydia Lydic, ila tetezi ya kutoka kwenye klabu ya Lydia Lydic inasema kwamba niko na mtaba nao wa miezi 4 na nimerudi hapa Bujumbura kwajili wanioneshe iyo Contrat (mkataba) kama imesainiwa na nani.
 shirikisho la soka la hapa Bujumbura tayari limekwisha ingilia kati na Raisi wa soka ya hapa Burundi Mheshimiwa Reverien amemuahidi kwamba mambo yote itakuwa sawa ila kitu cha muhimu ni makubaliano kati ya pande 2 endapo kama klabu ya Kenya inamuhitaji itakuja hapa Burundi ao itaandika barua yakuonesha wazi kama inataka kumusajili na wapate kuelewana na Lydia Lydic.
 kwa sasa msambuliaje kitegemeo wa Lydia Lydic yupo hapa Burundi ili kumaliza tatizo yake na aweze kujielekeza kenya na kucheza ligi ya kimataifa ya Kenya.


basi kama ombi tu ya worldnewz inaomba viongozi wa Lydia Lydic waweza kumurahisishia kijana wetu ajiendeye kucheza ligi ya kulipwa bali ya kukaa hapa na kupokea laki 2 kila mwaka ni aibu sana kwa mchezaji kama Fiston acheze kwenye Klabu bila mkataba wowote.
 hawa wachezaji 4 ndio wameonekana kama vitegemeo na kutafutwa kwenye ma klabu mbali mbali za inje ya nchi ya Burundi na baadhi ya Ferre , Lucio na Selemani wamekwisha sajiliwa na wamekwisha ondoka na kujiunga na klabu zao ambazo zimewasajili.

Maoni 2

Bila jina alisema ...

Imperialisme à la Burundaise,ayo mambo tunayajuwa sana, tena ni aibu sana kuona watu kama Gisage,Lydia na wengine waweze ku exploiter watu ivo.c'est vraiment honteux.kwa ajili ao watu hawa wapi watu thamani ya ki bin adam,Fiston akienda Kenya,atakuwa na uwezo wa kusaidiya familiya yake ata na taifa.

Bila jina alisema ...

200000fbu=120$/12=10$ kwa mwezi kama mshahara wa mchezaji kama Fiston.
Ata Federation inakubali watu wa exploiter wachezaji namna hiyo?mchezajin kama Fiston,Uvira (DRC) anaweza kupata 50$ kila akicheza,na anaweza pewa na watu binafsi 100$ na kazalika bila shida yoyote,kwa kila match.