MISHE-BOY

Tambwe Amissi Ama zangu ama zao

ni mchezaji wa vital'o ivi karibuni amesajiliwa na Klabu ya Simba kutoka Tanzania, katika maongezi yake ya kwanza hapo nchini Tanzania na amesema kuwa kama mtisha fulani: “Unajua nimewasoma wachezaji wa Tanzania hasa mabeki, wanatumia sana nguvu tofauti na kwetu Burundi, kule wanacheza mpira tu na ufundi mwingi.
tuwafahamishe kuwa ; STRAIKA mpya wa Simba mwenye uchu wa mabao, Mrundi Amis Tambwe amedai kuwa, ameshajua janja ya mabeki wa Tanzania na kwamba dawa yao ipo jikoni kwani yeye ni straika na shida yake ni kufunga tu.
Tambwe amesema kwamba mabeki hao wanatumia nguvu zaidi huku akisisitiza kuwa haogopi beki wala timu pinzani kwa sababu yeye ni kama askari jeshi anayekwenda kupigana vita, anachojua ni ushindi, hajui kama kuna kushindwa au kufa.


ufahamu kuwa,Tambwe alikuwa anaichezea Vital ‘O’  ya hapa nchini  Burundi ameondoka huku akiwa ameacha mechi mbili za Ligi Kuu hazijachezwa lakini ndiye kinara wa mabao, amefunga mabao 21 na wa pili anayemfuatia ana mabao 13 kwa hiyo zawadi ya ufungaji bora ni yake kwa asilimia kubwa na kwamba anaisubiri akiwa Tanzania.
Lakini pia ni mfungaji bora wa Kombe la Kagame msimu huu baada ya kufunga mabao sita katika mashindano yaliyofanyika Juni mwaka huu huko, Darfur, Sudan.
Akizungumzia upinzani wa timu, Tambwe alisema: “Ligi ya Tanzania ni ngumu na hakuna timu dhaifu, zote sawa na ingawa sina uzoefu sana lakini naona uwezo wa Yanga hautofautiani na timu nyingine tulizocheza nazo.
 na Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah Kibadeni ‘Mputa’ amesifu kiwango cha Tambwe na kusema anatarajia Simba itavuna mabao mengi kutoka kwake na pia ninamatumaini ya kupata beki nzuri yenye akili(hapa anmzungumzia Kaze Gilbert a.k.a Demunga naye pia ni Mrundi amesajiliwa na Simba pamoja na Mwenzie Tambwe).


 


Hakuna maoni