MISHE-BOY

DIDIER KAVUMBAGU KUWEKA RIKODI YANGA

 ni mchezaji mrundi ambae amewahi kuichezea klabu nyingi hapa nchini Burundi kwajina lake alisi ni DIDIER Kavumbagu , Kikosi cha Yanga, leo Alhamisi kinaanza safari ya kurudi nchini kikitokea kambini Uturuki, lakini kati ya nyota anayerudi kishujaa ni Mrundi huyo, aliyeibuka mfungaji bora nchini humo.
tukumbuke kuwa Katika kambi hiyo ya Yanga, ambayo ilikuwa katika mji wa Antalya, kikosi hicho kilicheza michezo minne ya kirafiki na klabu mbalimbali za Ulaya, na kilifunga jumla ya mabao saba na kufungwa mawili, lakini Kavumbagu akafunga matatu kati ya hayo saba.
 na baadhi ya wenye wanamufaham hapa ni Nyota  mrefu kuliko wote katika kikosi hicho cha Yanga alifunga bao la kwanza katika mchezo wa kwanza dhidi ya Ankara Sekespor, wakati Yanga ikiibuka na ushindi wa mabao 3-0 na mengine yakifungwa na Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza.

Mshambuliaji huyo aliifungia timu yake tena bao moja wakati ikicheza dhidi ya Altay S.K ya Uturuki na jingine likifungwa na Okwi, wakati Yanga ikiibuka na ushindi wa mabao 2-0 kabla ya kufanya hivyo tena katika mchezo wa mwisho wakati timu hiyo ilipotoka sare ya mabao 2-2 na Simerq PIK ya Azerbaijan na jingine likifungwa na Mrisho Ngassa.
Kabla ya mchezo huo wa mwisho kikosi hicho kiliumana na KS Flamurtari ya Albania na kulazimishwa suluhu. Wakati Kavumbagu akiweka rekodi hiyo alifuatiwa na Okwi raia wa Uganda aliyefunga mabao mawili huku Kiiza na Ngassa wakifuatia kwa kupachika bao moja kila mmoja lakini Ngassa akiweka rekodi yake kwa kuwa mzawa pekee aliyefunga katika ziara hiyo.
Rekodi nyingine ambayo imewekwa na Kavumbagu ni kwamba nyota huyo amefunga mabao hayo matatu, yote ni mabao ya kwanza ya Yanga katika kila mchezo akifunga bao la kwanza dakika 10, mchezo wa pili dakika 46 na wa mwisho dakika 13, na kumfanya kuweka rekodi hiyo ambayo awali iliwahi kuwekwa na mshambuliaji Jerry Tegete, aliyekuwa mfungaji bora katika ziara ya timu hiyo katika mji huo msimu uliopita kwa kupachika mabao mawili.


Hakuna maoni