MISHE-BOY

News | Natacha kuachia wimbo mpya muda wowote?

Staa wa muziki wa Burundi Fleva, Mwana mama Natacha maarufu kama La Namba Natacha-Nomaa amewataka mashabiki zake wa muziki kukaa mkao wa kula kwa ajili ya ujio wa wimbo wake mpya kama zawadi kwa ma fans wa muziki.

Hitmaker wa mdundo "Duga" aliyomshirikisha msanii nyota wa DR Congo, Fally Ipupa, alipost picha akiwa studio na producer ule ule aliyeitendea haki "Duga", Amir Pro na kuandika maneno ya fuatayo kwenye akaunti yake ya Instagram:
Sifa kubwa mwana mama huyu anayo ni ya kutangaza muziki wa nchi yake kimataifa, uwezo alionao aliakikisha kuweka rikodi ya kipekee Afrika Mashariki ya kuwa mwana muziki wa kwanza kukubaliwa kuimba na nyota wa DR Congo, Fally Ipupa.

Haijalishi anapitia wakati gani lakini Natacha ni Bora kunako jukwaa kuliko msanii yeyote wa kike nchini Burundi, Kwa kweli bila kupepesa macho kwa Burundi msanii wa kike akuwahi kutokea sijaona alofikia level za Natacha.

Natacha anajua kutumia mwili wake akiwa stejini na ana mbinu nyingi ndio moja ya sababu wanamuita Queen of Stage.

Kwasasa anatarajia kuachia wimbo wake mpya huku hakufahamisha jina la wimbo na kama ataimba pekee yake. Haya ndio maswali mashabiki wanaendelea kujiuliza na jibu itapatikana kwenye blog yako hiyi endelea kufuatilia...

Hakuna maoni