MISHE-BOY

Kocha Niyongabo Amars anajiandaa vilivyo kwa Derby dhidi ya klabu pinzani sana Garde Fc


Klabu ya A.s.a.s Djibouti  Telecom  ya nchini Djiboutie, klabu hio inaongozwa na  kocha mrundi  NIYONGABO AMARS AKBAR inazidi kujiandaa kwa mechi kubwa ambayo ni Derby ya hapo nchini Djiboutie. Kocha Amars anazidi kuwapa wachezaji wake tizi za kumzibiti mpinzani ata awe na kasi ya hali ya juu. Habari kutoka Djiboutie inathibitisha kwamba mechi iyo ambayo inasubiriwa na watu wengi sana ifikapo jumamosi tarehe 07/03/2015 saa moja  kamili ya usiku (19h00') majira ya Djiboutie na ni saa kumi na mbili (18h00') majira ya Burundi. Garde Republique ndio klabu ambayo watapambana nayo siku ya jumamosi uku tiketi zimeanza kuuziwa leo na ifikapo kesho tarehe saba tiketi azitapatikana tena  uku watu wakiwa wengi  kila mtu anatamani kuona mechi iyo ambayo ndio klabu mbili kila mwaka zinamashabiki wengi na wanazidi kukimbizana kwa kuchukuwa ubingwa msimu huu wakati ASAS Telecom inaongoza na mpinzani wake Garde Republique ikichukuwa na fasi ya pili, Garde Republique kwenye ukurasa wake wa Kijamii imeta,gaza na kusema awajaridhika nanafasi ya pili na watafanya kila iwezekanavyo wapate na fasi ya kwanza inayo milikiwa na kalbu ya kocha Amars pia na mchezaji mrundi Nzokira Jeff.
Tukumbuke kuwa ASAS Djibouti Telecom ni klabu ya goli kipa wa zamani wa Vital'o Fc, Nzokira Jeff na mchezaji wa zamani wa Lydia Lidic Academic Andosango Freddy ambayo wanazidi kuaminika sana kwenye iyo klabu kwa umahiri wao na uzowefu mkubwa sana.
 
Nzokira Jeff

Nzokira Jeff amesikika na kusema kwamba: kwakweli tuko sawa tena sana kama unavyo nisikia na niko fiti sana kwa izi tizi kocha anatupa sioni kama klabu gani inaweza kutubabaisha labda mambo ya Mungu tu ila tuko tayari na tunazidi kumpongeza kocha Amars anazidi kutuimarisha kiwango fulani ambaco atujawahi kuona wala kufunzwa na ni bahati kubwa kwangu .

Andosango Feddy: Dah ni machi ngumu sana ma elfu za watu watafika uwanjani kwakushuhudia mechi iyo ila mi sina uoga wowote niko hapa kwa kupambana na ndio kazi yangu, na kocha ni kocha mkubwa ametufunza mbinu zote za kumzibiti mpizani.


Tizama picha chache wakiwa kwenye mazowezi ya kujiandaa vilivyo kwa classico Djiboutie
Kocha Armas na Freddy



Hakuna maoni