MISHE-BOY

Sport | Watu 5 waaga dunia nchini Angola baada ya mechi ya Primeiro de Agosto-TP Mazembe

Tarifa mbaya zaidi imejitokeza nchini Angola baada ya mchezo  kati ya Premeiro de Angosto na TP Mazembe (0-0).

Watu 5 ikiwa ni pamoja na watoto wawili walikufa Jumamosi huko Luanda(Angola) kwenye mechi ya kwanza ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa kati ya Premeiro de Agosto na TP Mazembe. Wiki moja baada ya msiba huko Madagascar katika mechi ya mtoano ya CAN 2019 (Shabiki moja aliuawa katika vurugu ilijitokeza), mpira wa miguu la bara la Afrika inaendelea kuomboleza.

Hakika Wizara ya Vijana na Michezo ya Angola (MINJUD) ilitangaza Jumapili kuwa watu watano, ikiwa ni pamoja na watoto wawili, waliuawa Jumamosi baada ya mechi ya kwanza ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa kati ya  Primeiro de Agosto na TP Mazembe ( 0-0).

Tatizo bado haijulikani lakini palitokea na vurugu ya muda mfupi kwa mashabiki waliohudhuria mechi hiyo katika uwanja wa 11 Novemba wa Luanda, ambapo mchezo ulifanyika. Mechi hiyi ilivutiwa na watu wengi zaidi ya watu 50.0000.


Hakuna maoni